Tafuta katika Blogu Hii

Jumapili, 5 Julai 2015

JE KILA MTU ANAWEZA KUSAFISHA MAJI YA KISIMA AU BOMBA LAKE ?


Kama ilivyo leo kuna madaktari wengi ambao wamefungua vituo kwa ajili ya kutoa huduma za afya kwa jamii lakini si madaktari wote wamekidhi vigezo na masharti kwanza vya wao kuwa madaktari waliosomea fani hiyo ipasavyo na pili huduma wanayoitoa kwa wateja wao , kuibuka kwa wimbi la madaktari feki limekuwa tatizo kwenye sekta ya afya kwani wengi kwanza wamekuwa na gharama kubwa za matibabu kwa wateja na pia wakati mwingine kutoa maelezo yasiyo ya kweli kwa wagonjwa , pamoja ya kuwa kuna fulsa ya kujiongezea kipato kwa mtu kuwa na kituo chake cha huduma za afya lakini taaruma ni vema izingatiwe kuliko kujali pesa , vivyo hivyo ata kwenye suala la ubora wa maji lina taka ueledi na utaalamu ili kulinda afya za watu , nakumbuka wakati tuliokuwepo chuoni kimasomo mwalimu wetu aliyetufundisha somo la kutibu maji alituambia kuwa kama fundi sanifu katika maabara ya maji lazima uwe makini katika kuzingatia kiwango cha dawa kinachohitajika kwenye maji ili kupambana na vijidudu , alisema kuwa fundi sanifu anaweza kuua watu wengi kwa mda mfupi kuliko hata mwanajeshi anayetumia silaha vitani.
 




 

Mada hii nimeonelea ni vema nichapishe kwa sababu kuna mtu alishawahii kuja kuniuliza kuwa yeye maji yake ni machafu yakiwa na rangi inayoashiria uwepo wa madini ya chuma kwa wingi na turbidity(chembechembe ndogo za viasili vya kioganiki na vile visivyo vya kioganiki ) hivyo akaniambia kuwa aliwahi kununua shabu ikiwa kama mawe bila shaka ni aluminiam sulfate ili kuyasafisha maji hivyo alikuwa na nia ya kuweka ili asafishe kisima chake alitamani asikie sauti yamgu kama ningemluhusu aweke,  hapa ndipo lile swali ya kwamba kila mtu anaweza kusafisha maji yake linapopata jibu ya kwamba si kweli  hataukipewa kemikaliya klorini uweke kwenye maji ili kuua vijidudu haitashangaza kusikia umeua watu kwa sababu ya kutokuwa na utaalamu juu ya maji , hivyo lazime tuheshimu taaruma kuliko kujichukulia hatua mkononi binafsi naheshimu ninaposikia kuwa mtu katumia miaka kadhaa kusomea taaruma Fulani mfano nafahamu kuwa nikiumwa kichwa kuna dawa za kutuliza maumivu lakini unapokutana na daktari aliyetumia muda wake mwingi akiwa shuleni kusomea magonjwa ya mwanadamu huenda akaniambia tu wala nisitumie dawa ya kutuliza maumivu bali ninywe maji kwa wingi hivyo kichwa kitapona

 

HIVI NDIVYO UNAVYOTAKIWA KUFANYA MAJI YAKO YANAPOKUWA MACHAFU NA UKAHITAJI KUSAFISHA ILI KUUZA AU KWA MATUMIZI TU YA NYUMBANI

 

Nilimwambia mteja kuwa usijalibu kamwe kuweka hiyo dawa kwenye maji bali alitakiwa kuwaona mamlaka husika yaani wizara ya maji na mamlaka zinazotambulika hivyo lazima wangemwambia ni lazima sampuli ya maji yake ichukuliwe na kupelekwa maabara iliifanyiwe uchunguzi , pia angeambiwa na gharama ya kupima maji yake , na endapo taratibu zote zikifuatwa basi majibu yake yangekuja na ushauri nini kifanyike ili kuyafanya maji yake yawe salama na safi kwa matumizi

Njia hizo nimewahi kuzieleza kwenye mada inayosema  JINSI YA KUJUA MAJI NI SAFI NA SALAMA KWA MATUMIZI unaweza kuisoma na ukafahamu jinsi wataalamu watakavyo kusaidia

Endapo kama unahitaji maoni au ushauri juu ya maji unayotumia unaweza kunitumia barua pepe katika  mackthekwembe@gmail.com    

 

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni