Tafuta katika Blogu Hii

Jumapili, 28 Juni 2015


Maji yaonekanavyo inaweza kuchukuliwa kuwa hakuna shida au madhara yatokanayo lakini , madhara yake ni makubwa pale madini ya chumvi chumvi yanapo fanikiwa kuingia kwenye  mitungi ya machemshio   kiasi kwamba kiwanda kinawaza kufungwa  au ikagharimu pesa nyingi kuhakikisha uzalishaji unaendelea . 

Mitungi mikubwa ya kupozea au kuchemshia  hupatwa na athari za maji magumu pasipo kuangalia ubora wa hayo maji yanayotumika wakati wote hivyo ni jambo lisilohepukika


MADHARA YATAKAYOJITOKEZA PALE MAJI YENYE UGUMU  YATAKAPO TUMIKA KWENYE MACHEMSHIO

Pia maji ambayo hutumika kutengenezea au kuchanganyia dawa au kemikali kwa ajili ya kuzuia tatizo yanaweza kuchangia tatizo kama hhayaja safishwa vema

Kwa sababu maji yenye  ugumu hutokana na chumvi chumvi pale yanapotumika pasipo uangalifu hivyo ni vizuri kuwekeza kwenye teknologia ya maabara ya maji itakayosaidia kujua muonekano au ubora wa maji kabla hayajatumika  na yafuatayo ni madhara

  

Ca(HCO3)       +  JOTO              —›          H2O    +  CO2 (gesi)    +  CaCO3(Chanzo cha maji magumu au yenye chumvi chumvi)

 
 
 
 
 
 
 

kielelezo hapo juu ndio mfano halisi wa kile kinachotokea kwenye machemshio

 kalisiam kaboneti ndio mgando mgando unaojibandika kwenye kuta za machemshio na hivyo usababisha joto liwe kali sana kuliko inavyotakiwa lakini pia itakapotoke joto likazidi kupita kiasi machemshio yatakuwa mbioni kubutuka

 
Lakini pia majimagumu yatakapoachwa bila kutibiwa yatasababisha tabia ya kuzua joto lisisambae  maeneo yote ya machemshio


Tatizo lisipopatiwa ufumbuzi inaweza kuzuia ufanisi mzima wa mitungi ya kuchemshia  

 

NJIA ZA KUONDOA MAJI MAGUMU KABLA HAYAJALETA MADHARA

Kuna njia mbalmbali  za kuondoa chumvi chumvi za maji magumu  , nji ya kwanza ni kutumi kifaa kinachoitwa softener ambacho kina uwezo mkubwa wa kuondoa hizo chumvichumvi lakini kinatumika pale kabla maji hayajaingia kwenye mitungi ya kuchemshia

Mbali na softener tunaweza pia kutumia RO au reverse osmosis  ambapo kifaa hicho nacho huondoa kiasi kikubwa cha chumvi chumvi na kuzuia athari kabla ya maji kuingia kwenye mtungi wa kuchemshia

 

Njia nyingine ni kutumia chemikali ambazo zina phosphate au kaboneti ndani , polymers kama vile ctalized silphate  

 

Kama kuna jambo la kiteknolojia unaweza kuniandikia au kunitumia email ambayo ipo kwenye hii blogi

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni