Tafuta katika Blogu Hii

Jumapili, 22 Machi 2015

Maji Kama Rasimali Muhimu Kwako Yanakusaidiaje?

Maji ni rasilimali muhimu na ya pekee sana duniani na mahitaji yake ni makubwa sana , na matumizi yake pia ni makubwa  hivyo basi katika jamii yeyote ile inapotaabika na swala la kukosa maji , maisha huwa ni magumu sana kwa sababu tunahitaji maji katika mambo mengi sana ambapo sitamaliza nikitaja. Dhumuni kuu la blogu hii ni kuelimisha , kutoa ushauri juu ya matumizi bora ya maji na rasilimali zake, Kufanya utafiti juu ya fulsa mbalimbali zinazotokana na maji na pia kufahamu sayansi nzima ya maji katika matumizi mbalimbali  . Katika maisha yetu wanadamu maji huchukua sehemu kubwa sana, wataalamu wa masuala ya mazingira waliwahi kusema kwamba kuna siku ,Dunia itakuwa katika vita vya kugombania maji . Maji hutumika sehemu mbalimbali ikitegemeana na dhumuni la jamii husika , hivyo tunaweza kugawanya katika makundi ya fuatayo .



  1. Matumizi ya nyumbani
  2.  Matumizi ya viwandani
  3.  Matumizi kwa ajili ya umwagiliaji
  4.  Matumizi kwenye mapuli ya kuogelea .



1.MATUMIZI YA NYUMBANI

Nyumbani maaji hutumika kwa ,makusudi mbali mbali lakini muhimu zaidi ni matumizi kwa ajiri ya kunywa , hapa kila binaadamu anahusika matumizi mwngine ya nyumbani ni kama kupikia , kuoshea viombo , kufulia na hata kuogea  hivyo maji kwa matumizi ya nyumbani lazima yawe safi na salama , hasa kwa \ajiri ya kunywa maana ili tuishi lazima tunywe maji , pia tunahitaji maji mazuri ili tusimalize sabuni bila nguo tunazofua kutakata , na hata pale tuchemshapo maji yasiwaze kualibu viombo vya kupikia

Changamoto ni pale hatuwezi kukuta maji tunayoyatumia yako salama kwa matumizi hivyo ni lazima yasafishwe au kutibiwa ?



Njia au mbinu mbalimbali na juhudi za serikali zimekuwa zikifanyika kuhakikisha kwamba watu wanapata maji safi na salama ,

 Kuna matatizo na changamoto mbali mbali ambazo hukwamisha suala hili , na hasa kiuchumi  pale teknologia za kisasa zenye ufanisi mkubwa zinazo tumika nchi zilizoendelea huwa ni ndoto kwa nchi ambazo ndio zina endelea kama Tanzania jambo hil husababisha tujiwekee viwango vyetu wenyewe vya kupunguza madini ambayo hatuyahitaji kwenye maji. Viwango hivyo huwekwa na shirika la viwango nchini huwa si bora ukilinganisha na viwango vya kimataifa ambapo huwekeza pesa ya kutosha na hivyo kukuza teknologia yao .

Pia wakati mwingine siasa huchukua nafasi kubwa hata katika mambo yanayohitaji sayansi

 Wanasayansi wamegundua njia mbalimbali za kusafisha na kuondoa taka na vijidudu hatarishi kwenye maji yaliyo juu ya leya ya juu ya dunia nay ale yaliyo chini ya ardhi



Pia tatizo lingine ni kutothamini wataalamu walio katika sekta hii ya maji hasa watu wa vipimo vya maabara , ambao hufanya kazi katika mazimgira hatarishi hasa kwa afya zao




2            MATUMIZI YA VIWANDANI

..                                                                                                                                  

Matunizi ya viwandani



Maji hutumika viwandani kwa matumizi mbali mbali mfano vipo viwanda vinatumia maji kama malighafi katika utengenezaji wa bidhaa kama vinywaji , vyakula .

Maji pia hutumika viwandani kwa ajili ya kupoozea mitambo , tunajua wazi kwamba baadhi ya mitambo hupata joto kali hivyo maji ni kimiminika kizuli sana kwaajili ya kupooza mitambo hiyo

Tatizo hutokea pale maji ambayo yatatumika bila kuangaliwa ubora wake , hivyo husababisha mdhara makubwa kwenye mitambo hiyo , madhara hayo ni kama kujibandikiza bandikiza kwa madini Fulani kwenye kuta za mitambo , vilevile kubanduka au kukwanguka kwa hizo kuta za hiyo mitambo kwa sababu ya madini Fulani yasiyo hitajika mwisho wa yote hufanisi wake hupungua na kutofanya kazi ipasavyo , mfano kama viwanda vya kutengeneza sukari ambapo huingia gharama kubwa ya kutatua tatizo , au likiwa kubwa zaidi hutakiwa kuagiza mitambo mingine , hivyo kuepuka yote hayo ni lazima tuwe makini kwenye swala la ubora wa maji .

.



              3. MATUMIZI KWA AJILI YA UMWAGILIAJI



Maji yanaweza pia kutumika kwenye kilimo , lakini pia lazima yapimwe kujua kipi hakiitajiki kilichomo kwenye hayo maji ambapo kinaweza kuathiri mmea  hivyo ikasababisha hasara kubwa kwa mtu aliye wekeza kwenye kilimo





               4 .  MATUMIZI KWENYE MAPULI YA KUOGELEA



Maeneo mengi ya starehe na hasa kwenye mahoteli makubwa ambapo utakutana na mabwawa maarumu yaliyojegwa kwa ajili ya kuogelea , usalama na ubora wa hayo maji lazima uzingatiwe ili watumiaji wawe salama mbali na wadudu hatari kwenye maji , na hapa umakini huzingatiwa kwa sababu tu ya kibiashara



  Somo litakalofuata litaelezea  njia za kuondoa na kuua wadudu hatalishi-