Tafuta katika Blogu Hii

Jumapili, 24 Mei 2015

FAHAMU KUHUSU ‘PH” YA MAJI



                                              
  Watu wengi ujiuliza kwamba

PH ya maji ni nini  ?



PH ya maji ni neno la kikemia  hutumika kuwakilisha kupimo  cha asidiki au ukakasi kilichomo kwenye   maji ambapo kiasi hicho cha asidiki au ukakasi upimwa katika mfumo wa ayani zilizokuwa huru kwenye maji, nazo ni haidrogeni  ayani na zile za haidroksaidi ayani 





JINSI YA KUPIMA PH YA MAJI

1.PH ya maji inaweza kupimwa kwa kutumia kifaa maalumu cha kielekroniki kinachoitwa PH-mita  , kifaa hiki kina umbo dogo kiasi kwamba fundi sanifu anaweza kwenda nacho kwenye kituo cha kuchukulia sampuli na akaweza kupima akiwa huko .

















TAHADHARI KATIKA MATUMIZI YA KIFAA

Kifaa hiki ili kitoe majibu sahii ni lazima kikaguliwe kabla ya kutumika , watengenezaji wa kifaa hutoa kumbukumbu muhimu juu ya kifaa zitakazomsaidia fundi sanifu kukikagu juu ya usahii wake .



Kifaa hutumia kitambuzi ambacho ni elekrodi ili kupima kiwango cha ayani kwenye sampuli ya maji , hivyo ni muhimu kukikagua na kukisafisha kila baada ya matumizi lakini mfano wa kitu laini hutumika kusafishia elektrodi ili iwe katika hali ya kuhisi .  

PH- mita ,huifadhiwa kwenye kikasha maalumu kila baada ya kumaliza kukitumia



2. Universal solution . Hii ni chupa kubwa yenye  kemikali maalumu inayotumika kupima ph ya maji ikiwa na lebo inayonyesha rangi tofauti zilizopimwa katika kiwango fulani cha ph ikianzia 0 mbaka 14, kiwango cha vitone viwili  hudondoshwa kwenye kiasi cha mililita kumi hivi za sampuli ya maji, kisha rangi ubadilika kuendana na sampuli ya maji

ipo kwenye kiasi Fulani cha ph kwa kulinganisha na rangi zilizopo kwenye lebo ya universal solution .

  












Pia unaweza kupima PH kwa kutumia karatasi ndogo zinazopima PH ya 0 hadi 14 au inayoishia kwenye 12 , vikalatasi hivi huwa kwenye viboxi vidogo maalumu ambapo uchovywa kwenye
kiasi Fulani cha sampuli na kisha kulinganisha rangi iliyopangwa kitaalamu na ile ilyotokea .








Kwa nini tunahitaji kujua PH ya maji ?


Ni muhimu sana kujua pH ya maji kwasababu itatuambia kuwa nini kimezidi au kimepungua kati ya hali ya uasidi wa maji na hali ya ukakasi wa maji , mfano kwenye  maeneo ambayo maji ya kunywa yanayowekwa kemikali ya klorini ni muhimu kujua ph ya maji ambayo kiwango chake huwa kati 6.5—9.0 , kwa sababu maji hayo yanakuwa na visababishi vyote vya kupanda au kushuka kwa kiwango cha PH


Pia kuna kemikali mbali mbali zinazotumika kuzuia michubuko au kujibandikiza kwa solidi za kioganiki kwenye viwanda mabapo wana machemshio au vipoza mitambo ambapo maji yakiwa kwenye ph Fulani kemikali  hizo haziwezi kufanya kazi ipasavyo au ili tujue zimefanya kazi basi PH iwe katika kiwango fulani


PH ya maji ni miongoni mwa viwakilishi muhimu sana kuangalia kwenye maji , ikiwa unahitaji msaada wa kishauli usikose kunitumia barua pepe yangu yani mackthekwembe@gmail.com  au simu yangu ya mkononi kwa namba 0718746644 



Jumapili, 17 Mei 2015

JINSI YA KUJUA MAJI NI SAFI NA SALAMA KWA MATUMIZI





Unapotaka kujua kuwa maji yako yanafaa au hayafai kwa matumizi lazime kuzingatia kuwa ni nini kusudi la kutumia maji yako .Je ni kwa ajiri ya kunywa na matumizi ya nyumbani , kwa ajiri ya ujenzi , au kwa ajiri ya mapuli ya kuogela ?


Maji kabla hayajatua katika gamba la juu la dunia yakiwa kama mvua yanakuwa katika usalama ila pale yanapoifikia tu ardhi ndipo uhakika wa usalama wake ni sifuri , hii ni kwa sababu kuna mgusano wa mambo mengi ambayo yapo ardhini na maji yanapoifikia ardhi , mfano kuna madini mbali mbali kama vile aluminiam ,calcium na chembechembe za kioganiki , bila kusahau bacteria mbalimbali , ambao ukaa kwenye vinyesi vya wanyama damu moto mfano vibrio cholera . lakini ni mara ngapi tumewahi kuhisi au kuamini kuwa maji ya chanzo Fulani kama chemichemi ni safi na salama na wakati mwingine tumejalibu kunywa bila hata kuchemsha ?  hasa sehemu za vijijini watu wengi wamekuwa wakiishi kwa mazoea , hii imefanya ata kinga zao kukubaliana na mazingira ya maji wanayo yatumia , bila kuhisi kuumwa kwa muda mrefu , lakini angalizo ni kwamba , watu hao wapo kwenye hatari ya kuugua magonjwa yanayotokana na maji kama vile kipindupindu



Je tutajuaje sasa kuwa maji tunayoyatumia ni safi na salama ?

Hapa nitaelezea hatua za awali mbaka ile ya mwisho ambayo itatupatia hitimisho 



1 KUFAHAMU CHANZO CHA MAJI HUSIKA


Chanzo gani ambacho kina maji yanayotumiwa , chanzo kinaweza kuwa mto , ziwa au bwawa la kutengenezwa , kisima ,bomba la maji yakusambazwa au maji ya bahari , lengo la kujua chanzo kinaweza kutupa historia ya eneo husika , lakini kikuubwa zaidi ni ili tupate kuchukua sampuli ambayo itawakilisha chanzo kizima , pia tujue ni vifaa gani vya kwenda navyo kwenye kituo husika ili tuchukue sampuli ,neno sampuli humaanisha kiasi kidogo
cha kitu unakichukua kwaajiri ya kufanyia utafiti fulani lakini pindi utakapo pata jibu la kile unachokitafuta basi hiyo sampuli itawakilisha kitu kikubwa , mfano sampuli ya damu ya mnyama inaweza kuwa kiasi kidogo lakini ikawakilisha damu yote ya mwilini labda ikatolewa kwa ajili ya utafiti wa magonjwa, vivyo hivyo ni sawa na maji pia .






2       UCHUKUAJI WA SAMPULI ZA MAJI


 Katika kuchukua sampuli ya maji kunatofautiana kutokana na aina ya chanzo cha maji mfano  jinsi utakavyochukua sampuli ya maji ya mtoni ni tofauti na vile utakavyochukua sampuli ya kisima , pia hata ile ya bombani ,pia kuna chupa maalumu za kubebea sampuli nazo chupa hutofautiana ikitegemea nini kitakachoangaliwa kwenye maji ya chanzo husika mfano utakapo chukua sampili ya maji ili kujua kiwango gani cha hewa ya oxigeni kilichotumiwa na bacteri ili kuvunja vunja vitu vilivyooza ni lazima chupa yake iwe isiyopitisha mwanga wa jua ili kuzuia bacteria wasifanye kazi ndani ya maji hapa sitaelezea jinsi ya kuchukua sampuli ya vyanzo mbali mbali bali itakuwa ni mada itakayojitegemea wakati mwingine , lakini mkazo hapa , ili kupata majibu yaliyo sahii ni vema kuzingatia njia za uchukuaji wa sampuli na si kila mtu anaweza kuchukua sampuli bali ni mafundi sanifu wa maabara au mtu aliyepata mafunzo maalumu , baada ya kuchukua sampuli husika ni vema kukumbuka kufunga vifuniko vya chupa vizuri ili kutoruhusu kitu tofauti cha nje kuingia na pia kwa usalama wa sampuli isije kumwagika wakati wa safari ya kurudi











3       KUBANDIKA LEBO KATIKA KILA SAMPULI


 Ni kitu muhimu sana kubandika lebo katika kila chupa ya sampuli iliyokusanywa , hapa lebo itaonyesha ni muda gani sampuli ilichukuliwa na tarehe , chanzo cha sampuli mto bomba au kisima , jina la mtu aliyechukua sampuli , na mwisho kama sampuli inahitaji kutunzwa kwenye mazingira fulani ili isije kupoteza uhalisia wake











      4.  SAMPULI KUFIKISHWA MAABARA ILI ICHUNGUZWE


Hapa kabla sampuli ya maji haijachunguzwa  lazima isajiliwe , kuwa inatoka wapi , ni aina gani ya chanzo cha sampuli , pia nini kinachotakiwa kichunguzwe kwenye hiyo sampuli


Hapa sampuli ukutana na watu wengine tofauti walioajiriwa kwa kazi hiyo ya kusajiri sampuli na uwenda ikapewa namba ya utambulisho ili majibu yatakapo patikana yapelekwe mahali sampuli ilipotoka ili kuzuia kuchanganywa


Baada ya kusajiliwa kwa sampuli ,ni lazima maabara iwe tayali kwa ajili ya kufanya uchunguzi , hapa lazima wawepo mafundi sanifu ambao watabaki pindi wengine walipoenda kuchukua sampuli ili kuweka maabara katika hari safi na ya usalama ili kufanya kazi , mfano vifaa , vitakavyotumika viwe kwenye usafi na visivyo na matatizo , pia chemikali ziwe zimestandadaiziwa vizuri , sampuli upimwa kwa umakini ilikujua nini kilichomo au kinachokusudiwa , zipo njia mbili kuu zitakazotupa majibu ya kile tunachokitafuta katika maabara , yaani


·   Kutumia vifaa vinavyotoa majibu kidigitari


·   Na ile inayohusisha titresheni ambapo kemikali   huusika sana


Ingawa kwa uchunguzi wa kibailogia huwa tofauti na njia hizo kuu mbili , kwa sababu husisha kuotesha wadudu hivyo majibu upatikana kwa kila sampuli ingawa majibu mengine yanaweza kuchukua siku zaidi ya moja kwa kuwa wadudu wanaoteshwa kwa kupewa chakura Fulani , na katika jotolidi Fulani










5. ULINGANIFU WA MAJIBU NA VIWANGO VYA NCHI HUSIKA AU VYA KIMATAIFA


Baada ya maji kupimwa kitaalamu na kwa umakini mkubwa majibu yatakayopatikana ni lazima yalinganishwe na viwango vya nchi husika au vya WHO yaani kimataifa hii ni kutoka na ukweli kwamba si kila nchi inaweza kufiti viwango vya kimataifa kutokana na hali ya uchumi , ingawa utagundua kuwa viwango vya kimataifa vimejitahidi mno kupunguza athari au madhara yatakayo tokana na kemikali zitakazo onekana katika maji


Ukilinganisha na zile za nchi husika . hivyo baada ya kugundua kuwa maji yamekidhi viwango au la hatua ifuatayo ndio itakayohitimisha zoezi zima.



6. KUTOA RIPOTI



Katika hatua hii , ripoti itaandaliwa baada ya kulinganisha majibu tuliyopata na viwango vilivyowekwa mfano ikatokea kwamba kemikali zilizomo kwenye maji ni nyingi ukilinganisha na viwango vilivyowekwa basi fundi husika atatoa mapendekezo kuwa nini kifanyike , mfano kuweka dawa ili kuondoa lilichokuwemo au kutoa katazo kwamba maji yasitumike kabisa yanaweza kusababisho vifo au matatizo ya mda mrefu , baada ya hapo mteja atapewa majibu yake yenye ushauri jinsi gain afanye kutoka na ain ya maji anayotakakutumia .




Ushauri wangu hapa ni kwamba usitumie maji kwa mazoea , hasa matumizi ya kunywa kwa sababu gharama utakazotumia kujitibia zitakuwa kubwa zaidi kuliko pale utakapofuata ushauri wa wataalamu juu ya matumizi


Unaweza kuniandikia au kuomba ushauri juu ya aina ya maji unayotumia , kusudi lako husika , nami nitakushauri


Lengo la blogu hii ni kutoa elimu , juu ya sayansi ya maji na pia kusaidia jamii juu ya matumizi bora na sahihi ya maji ili yaweze kuwa uhai katika maisha yetu ya kila siku na vizazi vijavyo .









Alhamisi, 7 Mei 2015

IJUE KEMIKALI YA CHLORINE



Chlorine ni miongoni mwa elementi za kemikali zinazoaminika sana katika sayansi ya kutibu maji yaani kuua vijidudu hatarishi vya magonjwa katika maji, neno chlorine linatokana na neno la kilatini liitwalo chloros lenye maana rangi ya njano na ukijani kwa mbali hiyo ikiwa ni rangi ya gesi ya chlorine
Ni elementi ya 17 , katika chati ya mpangilio wa elementi , utaijua kwa alama hii (Cl),ikiwa katika kundi liitwalo halojeni,  uzito wa atomu yake ni 35.45g , pia inachemka katika joto la 34.04 nyuzi za sentigredi .
Chlorine inatabia ya kuchukuana na kemikali zingine kwa haraka sana  
Utofauti pekee unaoifanya kemikali hii kuwa bora katika sayansi ya kutibu maji ni kutokana na ukweli kwamba ikiyeyuka katika maji huwa katika mfumo wa kusafiri ikishambulia bacteria waliomo na watakaojitokeza kutokana na maji kukutana na vimelea vya nje vinavyoweza kupenya baada ya mpira wa kusafirishia maji kupasuka , vile vile chlorine hupatikana kilahisi na kwa gharama nafuu ;chlorine inapoyeyuka kwenye maji huwa katika mifumo miwili kitaalamu huitwa hypochlorite na hypochlrous acid hivyo huifanya iendelee kuwepo kwenye maji lakini pia atomu moja ya hydrojeni uondolewa na nitrogen atom uchukua nafasi pale chlorine inapo chukuana na ammonia ambayo ni miongoni mwa gesi zinazokuwepo kwenye maji , hii utokeza chloramines ambazo ni monochloramine , hypochloramine na tetrachloramine , hii uongeza ufanisi wa chlorine kuua vijidudu.








JINSI CHLORINE INAVYOFANYA KAZI
Chlorine inapokuwepo kwenye maji ambapo huwa na  bacteria , huwa  inaenda moja kwa moja kwenye ukuta wa seli wa mdudu na kualibu ukuta huo kisha utawala shughuli zote za hiyo seli ikiua na kutoruhusu mwendelezo wa kizazi wa hiyo seli .
Katika sehemu nyingi ambapo maji hukusanywa kutoka kwenye chanzo chake mfano , mito na hata maziwa ambapo maji hayo husukumwa kwa msukumo Fulani ikitegemea na geografia ya mahali husika hufikishwa sehemu maalumu (treatment plant) , ambapo kunahatua kadhaa maji hupitia kabla ya kuwekwa chlorine , hatua hizo zimeelezwa kwenymakala inayosema  hivi ndivyo maji yenye taka yanavyopitia mfumo wausafishwajikablahayajatumika,
JINSI CHLORINE INAVYOPATIKANA
Kemikali ya chlorine hutengenezwa na makampuni mbali mbali , na upatikana chini ya ardhi ndani ya baadhi ya miamba kemikali hii inaweza kuwa katika hali tofauti tofauti kama vile gesi yabisi na ata kimiminika ,kuna makampuni mengi yanayohusika katika kusambaza na kuuza chlorine ikiwa katika asilimia tofauti,pia ata ubora utofautian hivyo  , na asilimia za malighafi iliyomo mfano utaikutasodium yhpochlorite yenye asilimia 60 kutoka India .
Kiwango cha kemikali hii huwekwa kitaalamu kwenye maji na mafundi sanifu wa maabara ambapo ni lazima kiwango kinachowekwa kiendane na ujazo wa maji yatakayo tibiwa au ikitegemea viwango vya nchi tulivyojiwekea ili isizidi sana au pia isipungue .

MADHARA YA CHLORINE 
Chlorine ina madhara makubwa kwa mwanadamu hasa mtu anapoivuta kama gesi , kihistoria kuna vita iliyopiganwa na watu walitumia chlorine kama silaa , hata juzi tulisikia serikali ya nchi ya syria ikituhumiwa kutumia  gesi ya chlorine dhidi ya waasi , pia siku hadi siku chlorine inamadhara mtu anayefanya kazi pamoja nayo
Chlorine hualibu hasa mapafu , pia mtu anapoimeza kwa kiasi Fulani ukaa ndani ya mwili kwa muda mrefu ikitengeneza athari za kudumu, hivyo ata maji tunayokunywa si kila mtu anaweza kujimiminia tu chlorine kwenye kisima chake kwa kiasi anachotaka bali lazima kuwe na wataalamu wanaofahamu kiasi cha chlorine kinachohitajika , kiwango cha chlorine kisizidi  gramu tano , na chlorine inayosafiri baada ya ile inayohitaji kuwekwa intakiwa isizidi 0.2-0.3 kipimo katika mili lita ,


MAMBO YA KUJUA KUHUSU CHLORINE KABLA YA KUWEKWA KWENYE MAJI

Kitaalamu kemikali hii inapowekwa kwenye maji ni lazima kujua mambo matatu  muhimu ambayo ni
·         Chlorine iliyowekwa
·         Chlorine inayohitajika
·         Chlorine itakayobakia

Jambo hili ni la muhimu sana kwa sababu lazima kuwe na kiwango Fulani cha chlorine kibakie kwenye maji ukiachiliambali kile kilichohitajika na hayo maji , ili kusaidia kuua vijidudu hatarishi kutokana na ukweli kwamba maji yatakayosambazwa hupitia sehemu mbalimbali ambapo kupasuka kwa mipira ya kupielekea maji ni jambo la kawaida hivyo basi itasaidia kumaliza vijidudu vitakavyoingia baada ya mipira hiyo kupasuka

CHLORINE ILIYOWEKWA = CHLORINE INAYOHITAJIKA  + CHLORINE ITAKAYOBAKIA


JINSI YA KUSAFIRISHA CHLORINE

Ktokana na ukweli kwamba chlrine ina react kwa haraka sana hivyo husafirishwa kwa ungalifu wa hali ya juu sana isije ikaleta madhara , hivyo ufungwa kwenye mtungi mikubwa na kwa uhakika  usafiri kwa njia ya treni . ,
Usiache kuacha au kutuma maoni yako , maswali , juu ya maji au kiwanda chako kinavyohitaji au kutumia maji katika uzalishaji kupitia barua pepe yangu ya