Tafuta katika Blogu Hii

Jumatatu, 27 Aprili 2015

KWA NINI MAJI NI UHAI ?







Mtu akikosa chakula anaweza kuishizaidi ya miezi 2 akinywa maji tu, bali mtuakikosa maji kwa wiki2 tu anaweza kupoteza uhai ,  mwili wa binadamu kwa sehemu kubwa ni maji , Fikilia vile maji maji ambayo yapo mdomoni pale mtu anapokula chakula ikiwa ni hatua ya awali kabisa katika mfumo wa usagaji chakula hali hii uletwa na tezi ambalo huitwa salivary

Pia maji maji yaliyopo katikati ya viungo vya miguu ambayo usaidia mifupa isisagike  pia maji maji hayo usaidia kusinyaa na kutanuka kwa miguu , na ata kuweka msawaziko katika mwendo
Maji pia utokeza sehemu kubwa sana ya damu ambapo oxygen uweza kusafiri ikiwa kwenye mishipa midigo midogo kwa ajili ya shuguri mbali mbali za mwili
Maji hayo katika  uashiria kuwa mwili wa mwanadamu ni  maji kwa kiasi kikubwa 


KAZI ZA MAJI KATIKA MWILI
Mara nyingi nimesikia matabibu na wadau wengi wa sekta ya afya wakisisitiza watu kunywa maji angalau lita tano kwa siku , kutokana na watu wengi hapa duniani tumetingwa na shughuri nyingi hivyo huwa tunajisahau na kujikuta tukinywa kiasi kidogo sana cha maji matokeo yake tumejihisi wagonjwa na hata wengine kukimbilia hospitali kumbe ni kwamba atujazingatia kunywa maji mara kwa mara .

Mada ya hii itazungumzia kazi mbalimbali za maji katika mwili

  1. Maji usaidia kumeng’enya chakula katika mwili
Baada ya kumaliza kula tunahitaji maji , hii ni kwa sababu maji huusika moja kwa moja kusaga chakula , mbali na mmeng’enyo ambao hufanyika maji pia upeleka viini lishe mbalimbali ambavyo huitajika na seli za mwili kuusaidia mwili katika ukuaji au kuboresha zaidi pia maji usaidia kupata choo .

2 . Maji usaidia kuleta msawaziko bora wa kiasi cha joto la mwili
Kwa wastani joto la mwili wa mwanadamu ni 98.6 degree za falenhite au 37 degree za sentigredi , kutokana na shughuli mbali mbali za mwili kiasi cha joto kinaweza kupanda au kushuka , mfano mtu mwenye ugonjwa wa malalia joto lake la mwili linaweza likapanda sana au kupungua , hii kibailogia utokana na seli nyeupe zinazolinda mwili kuzidiwa nguvu na virusi vya ugonjwa hivyo mgonjwa ni lazime anywe maji ya kutosha ili kurekebisha joto la mwili .



3Maji ni muunganiko wa molekuli mbili yaani oxygen na hydrogen ambapo oxygen huitajika na ubongo kwa ajili ya shughuli zake za kila wakati , hivyo basi ili ubongo  uweze kufanya kazi vizuri unahitaji oxygen ambayo utokana na maji tunayokunywa Wakati mwingine tunaweza kuhisi dalili ya kwamba ubongo unahitaji oxygen pale tunapohisi maumivu ya kichwa wengi ukimbilia kutafuta dawa za kutuliza maumivu lakini mimi nashauri watu wajiulize kama walikunywa maji ya kutosha , ingawa si maumivu yote ya kichwa sababu huwa ni kukosa maji .                                                            
4 Maji pia usaidia figo katika kuchuja uchafu na sumu mbali mbali ambapo utolewa nje baada yo uchafu huo kuingia kwenye kibofu cha mkojo  ambapo ni miongoni mwa shughuli za mwili zinazohusisha seli hai .
Unaweza kujua pia kuwa mwili unahitaji  maji pale unapo enda aja ndogo na ukagundua kuwa mkojo umekuwa wemye rangi ya njano naharufu kali

Zote zilizotajwa ni faida za msingi za maji katika kuendeleza uhai wetu hivyo kuna
madhara mengi tutakayo kutana nayo pale tutakapo kosa kunywa maji kwa kiwango kinachotakiwa , mfano kujisikia uchovu , kuumwa kichwa na kukosa choo .
lakini changamoto leo ni je maji yako ni safi na salama ? na kama una uhakika  je utajuaje  ?  ,Ndani ya blogu hii utapata elimu ya kutosha kuhusiana na maji .


Ijumaa, 17 Aprili 2015

JE KWANINI MAJI YA BAHARI YANACHUMVI NYINGI ?



Maji ya bahari hutokana na mkusanyiko wa maji toka vyanzo mbali mbali kama mito , maziwa na ata maji yalioifikia bahari baada ya mvua kunyesha ,




  • Watu wengi wamekuwa wakijiuliza kuwa chumvi nyingi iliyopo katika bahari inatokana na nini hasa?  Mada hii itazungumzia hasa sababu za msingi zinazochangia uwepo wa madini ya chumvi katika bahari napenda kuongelea hili kwa sababu , pindi maji yakitoweka duniani au kupungua je kutakuwa na uwezakano wa kuyatumia ?  zipo nchi ambazo zimefanikiwa kwa kiasi Fulani kupunguza kiasi cha chumvi toka baharini na kuyatumia maji hayo kwa shughuri mbalimbali , pamoja na hayo gharama ya kuyasafisha maji hayo ni kubwa mno ukilinganisha na maji toka vyanzo vingine.

 

Si rahisi kwa maji ambayo yapo juu ya gamba la juu la dunia(fresh water) ambayo yametokana na kunyesha kwa mvua kuingia bahalini na kutokeza chumvi chumvi  kuna njia za msingi tatu ambazo zimeonekan kuwa ni sababishi za uwepo wa chumvi nyingi baharini na miongoni mwa njia hizo zimekuwa za asili hivyo sio rahisi kwa wanasayansi kuzuia visababishi,na hali hii imepelekea pia kiasi cha chumvi ya bahari kiwe kisicho badilika miaka nenda miaka rudi .



Zifuatazo ni njia zinazo ongeza chumvi katika bahari



  1. Kuwepo kwa maozo ya vitu mbalimbali vya asili kama vile wanyama , miti pia shughuri za kibinadamu hasa taka zinazozalishwa uchangia kwa kiasi Fulani , kuna viumbe vya asili vilivyo ozea  ndani ya bahari na vile vilivyoletwa na maji ya mito au maziwa baada ya kuingia baharini  



       2.Baada ya mvua kunyesha au maji yaliyotuama juu ya gamba la dunia hupenya nakuingia ndani ya miamba ambayo huwa na nyufa , nyufa hizo hutokea pale gamba la    ndani la dunia kupata msukumo mzito au mvutano wa asili , maji yanapoingia ndani ya miamba kazi yake kubwa ni kuyeyusha madini yaliyomo ndani ya miamba hiyo miongononi mwa hayo madini huwa ni chloride ambapo huwenda maji yalibeba madini mengine ya sodiam hivyo yanapoungana hutokeza chumvi ya nyumbani (sodiam chloride)

Na hivyo bahari kuwa na chumvi .

Kitu kingine cha kujua ni kwamba ipo mito inayosafiri chini kwa chini nayo huchangia uwepo wa chumvi kama ile mito iliyopo gamba la juu ya uso wa dunia(earth crust)



Yapo pia maziwa ambapo uchangia kuwepo kwa chumvi katika bahari hii ni si ali ya kawaida lakini maziwa hayo ni machache duniani mfano bahari nyekundu , kinachotokea katika maziwa ya kawaida ni kwamba , mito huingia kwanye maziwa nayo yakiwa yamebeba kiasi Fulani cha chumvi ambapo maziwa hayo hupokea maji na kuyatunza kwa muda kisha hutokeza njia ambapo mito hujirudia tena , na hivyo chumvi hupotea kutokana na mzunguko huo , lakini maziwa yenye kiasi kikubwa cha chumvi yenyewe hupokea maji ya mito lakini huwa hayana vinjia vitakavyofanya maji yarudie mito na kuendeleza mzunguko bali maziwa haya hujifanya bahari kwa kusubiri mbaka jua lichemshe maji na mvuke kwenda angani au kupotea hewani , kitendo hicho usababisha chumvi nyingi kubakia katika maziwa hayo .







3        Sababu hii haijatofautiana na ile ya pili isipokuwa hapa huusisha volcano inayotokea baadhi ya sehemu hivyo gamba la chini la dunia huwa kuna joto kali mno ambapohusababisha fukuto la uji wa moto , uji huo ni mkusanyiko wa madini yaliyoyeyusha na maji ya moto ikiwemo chloride ambayo ndio mama wa kutokeza chumvi , hali hii inapotoke huifikia bahari na kuchangia uwepo wa chumvi baharini




Nahitimisha mada hii kwa kusema chumvi ya bahari ni asili yake  kuwepo na kiwango chake akiongezeki wala kupungua ingawa bahari inauwezo wa kijisafisha yenyewe , inawezekana kupunguza chumvi kutoka maji ya bahari pale utakapotaka kuyatumia maji hayo , kama kwenye mapuli ya kuogelea , mada zijazo ntaongelea njia hizo .




Jumatatu, 6 Aprili 2015

HIVI NDIVYO MAJI YENYE TAKA YANAVYOPITIA MFUMO WA USAFISHWAJI KABLA HAYAJATUMIKA



Hapa nitazungumzia maji tunayotumia kila siku kwa matumizi ya nyumbani .
Nchini Tanzania maji tunayotumia hutokana na vyanzo mbali mbali vya maji hasa mito na maziwa , pia kuna mabwawa ya kutengenezwa  mfano bwawa la mindu ambapo pia bwawa hilo hutegemea sana maji kutoka kwenye mito mbali mbali inayotililisha maji kutoka milima ya uruguru . Wizara ya maji ndio imepewa jukumu kubwa hasa la kusimamia na kuendeleza vyanzo hivi kwa umuhimu w taifa letu kiujumla .
Hivyo wizara imegawanya vyanzo hivyo vya maji katika mabonde lakini mada hii haitazungumzia juu ya hayo mabonde .
Maji kutoka kwenye chanzo hubeba vitu mbali mbali ambavyo ndio taka  kama vile mizoga ya wanyama , miti iliyo angushwa na mvua au kwa nji yeyote , vinyesi vya wanyama akiwemo mwanadamu , uchafu kutokana na shughuli mbalimbali za watu kama nyavu za uvuvi , nguo nguo ,  na hata vijidudu viletavyo magonjwa na ata utupwaji wa taka za viwandani .  

ZIFUATAZO NI HATUA ZINAZOFANYIKA ILI KUWEZA KUPATA MAJI YALIYO SAFI NA SALAMA

HATUA ZA AWALI


1 Maji hupita kwenye machujio makubwa au ya kwanza ambapo ukilejea kwenye utangulizi utagundua kuwa maji hubeba taka zenye ukubwa tofauti tofauti hivyo kazi kubwa hasa ya hayo machujio ya kwanza ,
Hivyo baadhi ya taka ndogo ndogo zinaweza kupenya .
Basi watalamu wa maji baada ya kuona hilo wakatengeneza machujio mengine ambapo zile takandogo ndogo zilizo pata nafasi ya kupenya kwenye machujio ya kwanza hapa zimezuiliwa hivyo hubakia chembechembe za taka ambazo  si rahisi kuzichuja kwa hivyo hatua ifuatayo itaonyesha jinsi ya kuondoa hizo chembe chembe za taka



2.Kitaalamu inaeleweka kwamba chembe chembe ndogo za uchafu hubeba chagi hasi hivyo ili tuweze kuziondoa tunahitaji chagi chanya ambapo kitaalamu huitwa coagulant
Kwa hiyo coagulant ni kemikali inayowekwa kwenye maji ili kuungana na chembe ndogo ndogo za uchafu zenye chagi hasi , mfano wa hizo chemikali ni kama Alum au alminuam sulfeti pia ipo nyingine huitwa algae floc ,

3. Hatua hii husisha tanki ambalo linaluhusu maji yetu pamoja na coagulant vipate kuchanganyika na kitendo hicho usababisha chagi hasi na chanya ziungane na kutengeneza mabonge mabonge ya muungano hali hiyo huleta uzito hivyo madonge hayo hushuka chini kabisa ya tanki(basin) ambapo kitaalamu tunasema settlement .
Maji yetu hujitenga mbali na hayo madonge na kuonekana yenye utulivu  kwa juu

HATUA ZA UPILI
 4.Tunanahitaji maji yaweze kujitenga mbali na madonge yaliyo jitenga chini kabisa ya tanki hivyo hatua hii huitwa hatua ya mchujo (filtration) ambapo mji yetu hupelekwa kwenye tanki lingine ambapo kuna vichujio vinavyo husisha leya ya mchanga na leya ya grevos ambapo chembe ndogo za uchafu huchujwa  na madonge ambayo hutolewa na kupelekwa pembeni au dampo maalumu

5. Baada ya hapo maji yetu huonekana yako safi kwa ajili ya kutumia lakini hayapo salama kwa afya zetu kwa sababu bado yatakuwa na vimelea vya magonjwa, kama vile bacteria , virusi amiba nakadhalika , hivyo tunahitaji kuviondoa au kuviua ,hapa ndipo tunahitaji dawa ya kuyatibu maji yetu na kitendo hiki kitaalamu huitwa( disinfection)
Dawa inayoonekana kufanya vizuri zaidi hapa huitwa klorini ambayo inaweza kuwa katika mfumo wa gesi au kimiminika , ingawa mionzi inaweza kutumika kama vile ,
Ultravioleti na Ozoni ,lakini sababu kubwa inayofanya hii kemikali ya klorini iwe bora kuliko zingine ni kwamba inauwezo wa kubaki ikisafiri pindi maji yetu yanapoelekea kwenye jamii ya watumiaji , kwa sababu mipira ya kusambazia maji kuna wakati hupasuka maji yakiwa njiani hivyo  vijidudu hasa bacteria hupata nafasi nyingine ya kudhuru maji yetu hivyo kiasi kidogo sana na kilichopimwa kilicho kati ya mililita 0.2 hadi 0.5 cha dawa hushugulikia hivyo vijidudu .

6. Baada ya hapo maji yetu hupelekwa kwenye tanki kubwa sana ambalo huweza kumudu kubeba maji zaidi ya milioni elfu moja za lita kwa siku kwa ajili ya matumizi ya jamii husika
Hapo ndio mwisho wa jinsi ya kupata maji safi na salama kwa ajiri ya matumizi yetu ya kila siku , ingawa mfumo huu hugharimu kiasi kikubwa sana cha pesa katika kutengenezwa na kufanya ripea hivyo ni muhimu kufanya uangalizi wa mara kwa mara
 Uangalizi huusisha kusafisha machujio baada ya uchujaji kumalizika , kitendo hicho kitaalamu huitwa ( backwashing) tunahitaji kusafisha ili yasije yakaziba na kusababisha hasara na ufanisi usiotakiwa wa mtambo .

Pia uangalizi mwingine ni juu ya kiwango cha dawa ya klorini ambayo inatakiwa ibaki kwenye maji , harufu ya maji , na hata asidiki na ukakasi wa maji