Tafuta katika Blogu Hii

Ijumaa, 17 Aprili 2015

JE KWANINI MAJI YA BAHARI YANACHUMVI NYINGI ?



Maji ya bahari hutokana na mkusanyiko wa maji toka vyanzo mbali mbali kama mito , maziwa na ata maji yalioifikia bahari baada ya mvua kunyesha ,




  • Watu wengi wamekuwa wakijiuliza kuwa chumvi nyingi iliyopo katika bahari inatokana na nini hasa?  Mada hii itazungumzia hasa sababu za msingi zinazochangia uwepo wa madini ya chumvi katika bahari napenda kuongelea hili kwa sababu , pindi maji yakitoweka duniani au kupungua je kutakuwa na uwezakano wa kuyatumia ?  zipo nchi ambazo zimefanikiwa kwa kiasi Fulani kupunguza kiasi cha chumvi toka baharini na kuyatumia maji hayo kwa shughuri mbalimbali , pamoja na hayo gharama ya kuyasafisha maji hayo ni kubwa mno ukilinganisha na maji toka vyanzo vingine.

 

Si rahisi kwa maji ambayo yapo juu ya gamba la juu la dunia(fresh water) ambayo yametokana na kunyesha kwa mvua kuingia bahalini na kutokeza chumvi chumvi  kuna njia za msingi tatu ambazo zimeonekan kuwa ni sababishi za uwepo wa chumvi nyingi baharini na miongoni mwa njia hizo zimekuwa za asili hivyo sio rahisi kwa wanasayansi kuzuia visababishi,na hali hii imepelekea pia kiasi cha chumvi ya bahari kiwe kisicho badilika miaka nenda miaka rudi .



Zifuatazo ni njia zinazo ongeza chumvi katika bahari



  1. Kuwepo kwa maozo ya vitu mbalimbali vya asili kama vile wanyama , miti pia shughuri za kibinadamu hasa taka zinazozalishwa uchangia kwa kiasi Fulani , kuna viumbe vya asili vilivyo ozea  ndani ya bahari na vile vilivyoletwa na maji ya mito au maziwa baada ya kuingia baharini  



       2.Baada ya mvua kunyesha au maji yaliyotuama juu ya gamba la dunia hupenya nakuingia ndani ya miamba ambayo huwa na nyufa , nyufa hizo hutokea pale gamba la    ndani la dunia kupata msukumo mzito au mvutano wa asili , maji yanapoingia ndani ya miamba kazi yake kubwa ni kuyeyusha madini yaliyomo ndani ya miamba hiyo miongononi mwa hayo madini huwa ni chloride ambapo huwenda maji yalibeba madini mengine ya sodiam hivyo yanapoungana hutokeza chumvi ya nyumbani (sodiam chloride)

Na hivyo bahari kuwa na chumvi .

Kitu kingine cha kujua ni kwamba ipo mito inayosafiri chini kwa chini nayo huchangia uwepo wa chumvi kama ile mito iliyopo gamba la juu ya uso wa dunia(earth crust)



Yapo pia maziwa ambapo uchangia kuwepo kwa chumvi katika bahari hii ni si ali ya kawaida lakini maziwa hayo ni machache duniani mfano bahari nyekundu , kinachotokea katika maziwa ya kawaida ni kwamba , mito huingia kwanye maziwa nayo yakiwa yamebeba kiasi Fulani cha chumvi ambapo maziwa hayo hupokea maji na kuyatunza kwa muda kisha hutokeza njia ambapo mito hujirudia tena , na hivyo chumvi hupotea kutokana na mzunguko huo , lakini maziwa yenye kiasi kikubwa cha chumvi yenyewe hupokea maji ya mito lakini huwa hayana vinjia vitakavyofanya maji yarudie mito na kuendeleza mzunguko bali maziwa haya hujifanya bahari kwa kusubiri mbaka jua lichemshe maji na mvuke kwenda angani au kupotea hewani , kitendo hicho usababisha chumvi nyingi kubakia katika maziwa hayo .







3        Sababu hii haijatofautiana na ile ya pili isipokuwa hapa huusisha volcano inayotokea baadhi ya sehemu hivyo gamba la chini la dunia huwa kuna joto kali mno ambapohusababisha fukuto la uji wa moto , uji huo ni mkusanyiko wa madini yaliyoyeyusha na maji ya moto ikiwemo chloride ambayo ndio mama wa kutokeza chumvi , hali hii inapotoke huifikia bahari na kuchangia uwepo wa chumvi baharini




Nahitimisha mada hii kwa kusema chumvi ya bahari ni asili yake  kuwepo na kiwango chake akiongezeki wala kupungua ingawa bahari inauwezo wa kijisafisha yenyewe , inawezekana kupunguza chumvi kutoka maji ya bahari pale utakapotaka kuyatumia maji hayo , kama kwenye mapuli ya kuogelea , mada zijazo ntaongelea njia hizo .




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni