Tafuta katika Blogu Hii

Jumapili, 26 Julai 2015

REVERSE OSMOSIS

RO huondoa chembe ndogo ndogo za uchafu pale maji yanayosafishwa hupita katika kiwambo chembamba ambachokinaweza kuruhusu maji yakiwa pekeyake bila uchafu

Kinachotoke ni kwamba maji ambayo yana kiwango Fulani cha chumvi au madini mengine  husukumwa na msukumo mkali kupita kwenye kiwambo chembamba hivyo msukumo hupungua pale yanapo toka yakiwa katika hali bora

Vifaa vya RO huwa na uwezo wa kufanya kazi katika msukumo  wa kati ya 200  -  800 psig

 

Pia RO imetengenezwa kiasi kwamba maji yanatibiwa dhidi ya bacteria  kwa kutumia mionzi ya uv ingawa pia kiwambo chembamba kinachoruhusu maji yasiyo na chumvi iliyoyeyuka kupenya ina vitundu ambavyo vinaweza kutoruhusu bacteria kupenya hivyo wakaondolewa kwa njia ya kawaida
 
JINSI RO INAVYOFANYA KAZI

Mada iliyopita nilielezea maana ya RO hivyo hapa nitaelezea jinsi gani mtambo huu ufanya kazi , lengo langu ni kwamba msomaji wa blogu hii upate kuelewa kwa namna Fulani juu ya RO

Maji kutoka kwenye chanzo huingia kwenye maifazio na kisha kuruhusiwa kwenda kwenye mtambo ili kazi ya kusafishwa iweze kuanza  kitendo cha asili yaani osmosis huitaji maji yaliyo katika msukumo mdogo kwenda kwenye yale yaliyo na msukumo mkubwa yakipita kwenye kiwambo chembamba cha matilio maalumu ya kuchuja 

Neno reverse humanisha  kinyume hivyo kifaa hiki  uruhusu maji yenye mgandamizo mkubwa kwenda mdogo kwa msaada wa pampu ambayo usaidia katika msukumo na hivyo ndivyo maji yanapochujwa hivyo maji yenye mgandamizo mkubwa huelekea kwenye eneo lenye mgandamizo mdogo  hivyo msukumo mkubwa ndio utakao sababisha chumvi iliyoyeyuka iweze kuondolewa kwa kiwango kikubwa , wataalamu huamini kuwa RO inaweza kuondoa asilimia 95 hadi 99 za chumvi iliyoyeyuka

 

Pia ufanisi unapoonekana umepungua tatizo linaweza kuwa viwambo vyembamba vikawa vimezidiwa uwezo wa kuchuja au kuondoa chumvi iliyoyeyuka hivyo huitajika vibadilishwe

 

Jumapili, 12 Julai 2015

REVERSE OSMOSIS


RO ni kifaa cha kisasa kinachotumika kuondoa chumvichumvi ambayo hutokeza maji magumu  , mada zilizopita nilielezea madhara ya maji magumu

Kifaa hiki kimetengenezwa kiasi kwambwa kina uwezo wa kuvuta chuvi chumvi yote na kuyaacha maji yakiwa salama

Lakini  uwezo wa kuondoa chumvi hutofautiana kwa kifaa kimoja na kingine ikitegemeana na kiwango cha chumvi

Pia RO imetengenezwa kiasi kwamba maji yanatibiwa dhidi ya bacteria  kwa kutumia mionzi ya uv

 

 

Jumapili, 5 Julai 2015

JE KILA MTU ANAWEZA KUSAFISHA MAJI YA KISIMA AU BOMBA LAKE ?


Kama ilivyo leo kuna madaktari wengi ambao wamefungua vituo kwa ajili ya kutoa huduma za afya kwa jamii lakini si madaktari wote wamekidhi vigezo na masharti kwanza vya wao kuwa madaktari waliosomea fani hiyo ipasavyo na pili huduma wanayoitoa kwa wateja wao , kuibuka kwa wimbi la madaktari feki limekuwa tatizo kwenye sekta ya afya kwani wengi kwanza wamekuwa na gharama kubwa za matibabu kwa wateja na pia wakati mwingine kutoa maelezo yasiyo ya kweli kwa wagonjwa , pamoja ya kuwa kuna fulsa ya kujiongezea kipato kwa mtu kuwa na kituo chake cha huduma za afya lakini taaruma ni vema izingatiwe kuliko kujali pesa , vivyo hivyo ata kwenye suala la ubora wa maji lina taka ueledi na utaalamu ili kulinda afya za watu , nakumbuka wakati tuliokuwepo chuoni kimasomo mwalimu wetu aliyetufundisha somo la kutibu maji alituambia kuwa kama fundi sanifu katika maabara ya maji lazima uwe makini katika kuzingatia kiwango cha dawa kinachohitajika kwenye maji ili kupambana na vijidudu , alisema kuwa fundi sanifu anaweza kuua watu wengi kwa mda mfupi kuliko hata mwanajeshi anayetumia silaha vitani.
 




 

Mada hii nimeonelea ni vema nichapishe kwa sababu kuna mtu alishawahii kuja kuniuliza kuwa yeye maji yake ni machafu yakiwa na rangi inayoashiria uwepo wa madini ya chuma kwa wingi na turbidity(chembechembe ndogo za viasili vya kioganiki na vile visivyo vya kioganiki ) hivyo akaniambia kuwa aliwahi kununua shabu ikiwa kama mawe bila shaka ni aluminiam sulfate ili kuyasafisha maji hivyo alikuwa na nia ya kuweka ili asafishe kisima chake alitamani asikie sauti yamgu kama ningemluhusu aweke,  hapa ndipo lile swali ya kwamba kila mtu anaweza kusafisha maji yake linapopata jibu ya kwamba si kweli  hataukipewa kemikaliya klorini uweke kwenye maji ili kuua vijidudu haitashangaza kusikia umeua watu kwa sababu ya kutokuwa na utaalamu juu ya maji , hivyo lazime tuheshimu taaruma kuliko kujichukulia hatua mkononi binafsi naheshimu ninaposikia kuwa mtu katumia miaka kadhaa kusomea taaruma Fulani mfano nafahamu kuwa nikiumwa kichwa kuna dawa za kutuliza maumivu lakini unapokutana na daktari aliyetumia muda wake mwingi akiwa shuleni kusomea magonjwa ya mwanadamu huenda akaniambia tu wala nisitumie dawa ya kutuliza maumivu bali ninywe maji kwa wingi hivyo kichwa kitapona

 

HIVI NDIVYO UNAVYOTAKIWA KUFANYA MAJI YAKO YANAPOKUWA MACHAFU NA UKAHITAJI KUSAFISHA ILI KUUZA AU KWA MATUMIZI TU YA NYUMBANI

 

Nilimwambia mteja kuwa usijalibu kamwe kuweka hiyo dawa kwenye maji bali alitakiwa kuwaona mamlaka husika yaani wizara ya maji na mamlaka zinazotambulika hivyo lazima wangemwambia ni lazima sampuli ya maji yake ichukuliwe na kupelekwa maabara iliifanyiwe uchunguzi , pia angeambiwa na gharama ya kupima maji yake , na endapo taratibu zote zikifuatwa basi majibu yake yangekuja na ushauri nini kifanyike ili kuyafanya maji yake yawe salama na safi kwa matumizi

Njia hizo nimewahi kuzieleza kwenye mada inayosema  JINSI YA KUJUA MAJI NI SAFI NA SALAMA KWA MATUMIZI unaweza kuisoma na ukafahamu jinsi wataalamu watakavyo kusaidia

Endapo kama unahitaji maoni au ushauri juu ya maji unayotumia unaweza kunitumia barua pepe katika  mackthekwembe@gmail.com