Tafuta katika Blogu Hii

Jumapili, 14 Juni 2015

MAJI MAGUMU ( HARD WATER)


 

 Maji magumu ni maji ambayo yanapotumika kuoshea viombo au kufulia nguo hayawezi kutokeza povu , bali utaona utando mweupe ukielea juu , je hii usababishwa na nini ?

Maji magumu huwa yanakuwa na kiasi kikubwa cha madini ya chokaa, yanayotokana na metali za kalishamu na magniziamu , metali hizo uyeyushwa pale maji yanayotokana na mvua kupenya chini ya ardhi ambapo miamba yenye nyufa uruhusu maji yasiyo na madini kwenda kuyeyusha metali za chokaa na kusababisha maji yawe magumu

 
 

Maji haya yanaweza kuwa mahari popote ambapo kuna miamba yenye madini ya chokaa , yaani kalisiam kaboneti au magniziam kaboneti

 caco2(s)
 
 
 

MADHARA YA MAJI MAGUMU KWA WATUMIAJI
 
Maji magumu hayana madhara katika mwili wa mnyama au mwanadamu pindi atakapo yatumia maji hayo bali athari zake huwa ni kubwa zaidi kwenye viwanda ambapo bilakuwa makini na maji magumu . yanaweza kusababisha hasara kubwa inayotokana na kualibika kwa mitambo hiyo , pia maji magumu usababisha mitungi ya kuchemshia maji isiwe na kiwango kizuri cha kuhifadhi joto , athari huwa ni kubwa ata katika mitungi ya maji kwa ajiri ya kupozea  mitambo ,kutokana na utando mnene wa chokaa kujibandika kwenye kuta za mtambo uliotengenezwa na madini ya metali . .

 

 

 

 

      

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni