Tafuta katika Blogu Hii

Jumatatu, 27 Aprili 2015

KWA NINI MAJI NI UHAI ?







Mtu akikosa chakula anaweza kuishizaidi ya miezi 2 akinywa maji tu, bali mtuakikosa maji kwa wiki2 tu anaweza kupoteza uhai ,  mwili wa binadamu kwa sehemu kubwa ni maji , Fikilia vile maji maji ambayo yapo mdomoni pale mtu anapokula chakula ikiwa ni hatua ya awali kabisa katika mfumo wa usagaji chakula hali hii uletwa na tezi ambalo huitwa salivary

Pia maji maji yaliyopo katikati ya viungo vya miguu ambayo usaidia mifupa isisagike  pia maji maji hayo usaidia kusinyaa na kutanuka kwa miguu , na ata kuweka msawaziko katika mwendo
Maji pia utokeza sehemu kubwa sana ya damu ambapo oxygen uweza kusafiri ikiwa kwenye mishipa midigo midogo kwa ajili ya shuguri mbali mbali za mwili
Maji hayo katika  uashiria kuwa mwili wa mwanadamu ni  maji kwa kiasi kikubwa 


KAZI ZA MAJI KATIKA MWILI
Mara nyingi nimesikia matabibu na wadau wengi wa sekta ya afya wakisisitiza watu kunywa maji angalau lita tano kwa siku , kutokana na watu wengi hapa duniani tumetingwa na shughuri nyingi hivyo huwa tunajisahau na kujikuta tukinywa kiasi kidogo sana cha maji matokeo yake tumejihisi wagonjwa na hata wengine kukimbilia hospitali kumbe ni kwamba atujazingatia kunywa maji mara kwa mara .

Mada ya hii itazungumzia kazi mbalimbali za maji katika mwili

  1. Maji usaidia kumeng’enya chakula katika mwili
Baada ya kumaliza kula tunahitaji maji , hii ni kwa sababu maji huusika moja kwa moja kusaga chakula , mbali na mmeng’enyo ambao hufanyika maji pia upeleka viini lishe mbalimbali ambavyo huitajika na seli za mwili kuusaidia mwili katika ukuaji au kuboresha zaidi pia maji usaidia kupata choo .

2 . Maji usaidia kuleta msawaziko bora wa kiasi cha joto la mwili
Kwa wastani joto la mwili wa mwanadamu ni 98.6 degree za falenhite au 37 degree za sentigredi , kutokana na shughuli mbali mbali za mwili kiasi cha joto kinaweza kupanda au kushuka , mfano mtu mwenye ugonjwa wa malalia joto lake la mwili linaweza likapanda sana au kupungua , hii kibailogia utokana na seli nyeupe zinazolinda mwili kuzidiwa nguvu na virusi vya ugonjwa hivyo mgonjwa ni lazime anywe maji ya kutosha ili kurekebisha joto la mwili .



3Maji ni muunganiko wa molekuli mbili yaani oxygen na hydrogen ambapo oxygen huitajika na ubongo kwa ajili ya shughuli zake za kila wakati , hivyo basi ili ubongo  uweze kufanya kazi vizuri unahitaji oxygen ambayo utokana na maji tunayokunywa Wakati mwingine tunaweza kuhisi dalili ya kwamba ubongo unahitaji oxygen pale tunapohisi maumivu ya kichwa wengi ukimbilia kutafuta dawa za kutuliza maumivu lakini mimi nashauri watu wajiulize kama walikunywa maji ya kutosha , ingawa si maumivu yote ya kichwa sababu huwa ni kukosa maji .                                                            
4 Maji pia usaidia figo katika kuchuja uchafu na sumu mbali mbali ambapo utolewa nje baada yo uchafu huo kuingia kwenye kibofu cha mkojo  ambapo ni miongoni mwa shughuli za mwili zinazohusisha seli hai .
Unaweza kujua pia kuwa mwili unahitaji  maji pale unapo enda aja ndogo na ukagundua kuwa mkojo umekuwa wemye rangi ya njano naharufu kali

Zote zilizotajwa ni faida za msingi za maji katika kuendeleza uhai wetu hivyo kuna
madhara mengi tutakayo kutana nayo pale tutakapo kosa kunywa maji kwa kiwango kinachotakiwa , mfano kujisikia uchovu , kuumwa kichwa na kukosa choo .
lakini changamoto leo ni je maji yako ni safi na salama ? na kama una uhakika  je utajuaje  ?  ,Ndani ya blogu hii utapata elimu ya kutosha kuhusiana na maji .


Maoni 5 :

  1. Ni hakika maji ni muhimu kwa maisha binadamu kuliko tunavyodhani

    JibuFuta
  2. Maji ni uhai lakini ukizama baharini unakufa

    JibuFuta
  3. Maji ni uhai lakini ukizama baharini unakufa

    JibuFuta
  4. Maji ni uhai lakini ukizama baharini unakufa

    JibuFuta
  5. maji nikitu muhimu sana baada ya pumzi katika maisha ya kila kitu kiishivyo.

    JibuFuta