Tafuta katika Blogu Hii

Jumapili, 28 Juni 2015


Maji yaonekanavyo inaweza kuchukuliwa kuwa hakuna shida au madhara yatokanayo lakini , madhara yake ni makubwa pale madini ya chumvi chumvi yanapo fanikiwa kuingia kwenye  mitungi ya machemshio   kiasi kwamba kiwanda kinawaza kufungwa  au ikagharimu pesa nyingi kuhakikisha uzalishaji unaendelea . 

Mitungi mikubwa ya kupozea au kuchemshia  hupatwa na athari za maji magumu pasipo kuangalia ubora wa hayo maji yanayotumika wakati wote hivyo ni jambo lisilohepukika


MADHARA YATAKAYOJITOKEZA PALE MAJI YENYE UGUMU  YATAKAPO TUMIKA KWENYE MACHEMSHIO

Pia maji ambayo hutumika kutengenezea au kuchanganyia dawa au kemikali kwa ajili ya kuzuia tatizo yanaweza kuchangia tatizo kama hhayaja safishwa vema

Kwa sababu maji yenye  ugumu hutokana na chumvi chumvi pale yanapotumika pasipo uangalifu hivyo ni vizuri kuwekeza kwenye teknologia ya maabara ya maji itakayosaidia kujua muonekano au ubora wa maji kabla hayajatumika  na yafuatayo ni madhara

  

Ca(HCO3)       +  JOTO              —›          H2O    +  CO2 (gesi)    +  CaCO3(Chanzo cha maji magumu au yenye chumvi chumvi)

 
 
 
 
 
 
 

kielelezo hapo juu ndio mfano halisi wa kile kinachotokea kwenye machemshio

 kalisiam kaboneti ndio mgando mgando unaojibandika kwenye kuta za machemshio na hivyo usababisha joto liwe kali sana kuliko inavyotakiwa lakini pia itakapotoke joto likazidi kupita kiasi machemshio yatakuwa mbioni kubutuka

 
Lakini pia majimagumu yatakapoachwa bila kutibiwa yatasababisha tabia ya kuzua joto lisisambae  maeneo yote ya machemshio


Tatizo lisipopatiwa ufumbuzi inaweza kuzuia ufanisi mzima wa mitungi ya kuchemshia  

 

NJIA ZA KUONDOA MAJI MAGUMU KABLA HAYAJALETA MADHARA

Kuna njia mbalmbali  za kuondoa chumvi chumvi za maji magumu  , nji ya kwanza ni kutumi kifaa kinachoitwa softener ambacho kina uwezo mkubwa wa kuondoa hizo chumvichumvi lakini kinatumika pale kabla maji hayajaingia kwenye mitungi ya kuchemshia

Mbali na softener tunaweza pia kutumia RO au reverse osmosis  ambapo kifaa hicho nacho huondoa kiasi kikubwa cha chumvi chumvi na kuzuia athari kabla ya maji kuingia kwenye mtungi wa kuchemshia

 

Njia nyingine ni kutumia chemikali ambazo zina phosphate au kaboneti ndani , polymers kama vile ctalized silphate  

 

Kama kuna jambo la kiteknolojia unaweza kuniandikia au kunitumia email ambayo ipo kwenye hii blogi

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Jumapili, 21 Juni 2015

FAHAMU KUHUSU TDS KATIKA MAJI


                                                            
TDS  ni neno linalotumika kama msamiati na kifupisho cha maneno ya kiingereza yanayojulikana kama Total dissolved solids  ikimaanisha kuwa ndani ya maji ambayo yamekutana au kugusana na viwakilishi mbali mbali kama vya kiumbo , kikemikali au vya kibaiologia  hivyo TDS , huwakilisha mgusano wa maji na chembe chembe za uchafu zikijumuisha element au kompaundi mbalimbali za kikemikali zilizoweza kuyeyushwa na maji au zilizotengeneza mgando mgando kutokana maji kushindwa kuziyeyusha , hivyo basi chembendogo hizo zinakuwa na chaji chanya na hasi   pia TDS hujumuisha hata chumvi zisizokuwa za kioganiki

 
 

 

TDS hutuonyesha picha ya kwamba ni jinsi gani maji yetu yamechafuka au kukutana na uchafu ingawa ni ngumu kutupa jibu halisi la kiwango cha uchafuzi  hasa katika maji ya kunywa  hivyo mara nyingi tunapokuwatunapima mahabara  TDS hutupa picha ya kwamba majibu ya vipimo vingine yatakuwaje mfano TDS inapokuwa kubwa tunategemea pia chloraidi iwepo .

Kiwango kilichowekwa na EPA huko marekanni kuhusu TDS inatakiwa kisizidi milligram 500 katika lita yamaji                     

 

 

 

                                                           JINSI YA KUPIMA TDS KATIKA MAJI

Kwa sababu TDS hujumuisha chembechembe ndogo zilizo na chagi hasi na chanya hivyo huwa zinatembea zikigongana kwenye maji kila moja ambapo kitaalamu huita ions kwa jinsi hiyo njia ya kielekroniki hutumika katika kupima hizo chembe chembe zilizobeba chagi 
TDS hupimwa katika miligramu kwa lita moja (mg/l)
Wataalamu wametengeneza kifaa kinachoitwa TDS – Meter  ambacho hutumika katika kupimia

Kifaa hicho kimetengenezwa kiasi kwamba huwa na uwezo wa kuhisi kuwa kuna kiwango gani cha TDS lakini pia kuna mahusiano ya karibu sana kati ya TDS pamoja na EC neno EC hutokana na neno la kiingereza yaani electric conductivity ambapo humaanisha uwezo wa maji yenye chembechembe hasi na chanya kupitisha umeme huwezo huo upimwa katika microsemens per sentimita

 

Kifaa kwa ajili ya kupima TDS kimetengenezwa kuwa na uwezo wa kupima na EC pia . ingawa kinaweza kusomwa katika mtindo wa skeli au wa digitali ikitegemeana na watengenezaji wa kifaa husika walivyotengenezwa  , kifaa pia huwa na mahari penye kihisia  ambapo kiasi kidogo cha sampuli ya maji humiminwa ili kujua kiwango cha TDS na EC






 












Sampuli ya maji inaweza kutibiwa kwanza kabla ya kupima ikitegemea ni aina gani ya sampuli pia kifaa ni lazima kikaguliwe kama kipo katika ubora wake

Baada ya kukagua kifaa , kuwa kipo tayali kiasi kidogo cha sampuli kitamiminwa kwenye kifaa na kubonyeza kitufe cha kupimia ndipo jibu litaonekana katika mfumo wa digitari au wa skeli  ,

 

 

 

      

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

  

 

 

 

Jumapili, 14 Juni 2015

MAJI MAGUMU ( HARD WATER)


 

 Maji magumu ni maji ambayo yanapotumika kuoshea viombo au kufulia nguo hayawezi kutokeza povu , bali utaona utando mweupe ukielea juu , je hii usababishwa na nini ?

Maji magumu huwa yanakuwa na kiasi kikubwa cha madini ya chokaa, yanayotokana na metali za kalishamu na magniziamu , metali hizo uyeyushwa pale maji yanayotokana na mvua kupenya chini ya ardhi ambapo miamba yenye nyufa uruhusu maji yasiyo na madini kwenda kuyeyusha metali za chokaa na kusababisha maji yawe magumu

 
 

Maji haya yanaweza kuwa mahari popote ambapo kuna miamba yenye madini ya chokaa , yaani kalisiam kaboneti au magniziam kaboneti

 caco2(s)
 
 
 

MADHARA YA MAJI MAGUMU KWA WATUMIAJI
 
Maji magumu hayana madhara katika mwili wa mnyama au mwanadamu pindi atakapo yatumia maji hayo bali athari zake huwa ni kubwa zaidi kwenye viwanda ambapo bilakuwa makini na maji magumu . yanaweza kusababisha hasara kubwa inayotokana na kualibika kwa mitambo hiyo , pia maji magumu usababisha mitungi ya kuchemshia maji isiwe na kiwango kizuri cha kuhifadhi joto , athari huwa ni kubwa ata katika mitungi ya maji kwa ajiri ya kupozea  mitambo ,kutokana na utando mnene wa chokaa kujibandika kwenye kuta za mtambo uliotengenezwa na madini ya metali . .