Tafuta katika Blogu Hii

Jumapili, 16 Agosti 2015

CHANGAMOTO ZA MAJI TAKA KATIKA MAJIJI YANAYOKUWA


MAJI TAKA

Maji taka ni yale maji yaliyogusana na uchafu au kitu kisichohitajika kwenye maji , yakihusisha mkusanyiko kutoka mahali tofauti tofauti mfano nyumbani , maji yaliyotumika kuogea ,kufulia , kuoshea viombo na wakati mwingine yakihusishwa na uwepo wa vinyesi , pia maji haya yanaweza kutoka viwandani au kwenye taasisi mbalimbali .

Mkusanyiko wote wa maji haya taka hukutana katika bomba moja kubwa ambalo litasafilisha kuelekea kwenye kumwagwa au kusafishwa na kutibiwa ili yawe katika kiwango kisicholeta madhara kwenye mazingira

Kumekuwapo na changamoto juu ya haya maji taka hasa sehemu za  mijini,uwenda hata wewe ukawa mmojawapo kati ya wale waliokutana na kero ya kuona au hata kukanyaga maji haya machafu wakati ukiwa katika matembezi ,

Maji haya taka ni hatari hasa pale yanapokutana na mfumo wa maji safi ,ambapo  mipira ya kusambazia maji safi inaweza kupasuka hivyo ikapelekea athari kubwa kwa watumiaji    


 

SABABU ZA MAJI TAKA KULETA KELO MIJINI

Hapa kuna sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili sahemu za mijini ingawa wapo wanasiasa wanaodai kuwa inatokana na ujenzi unaondelea kila kukicha katika miji mikubwa hasa ujenzi wa majengo marefu , sitaki kusema sio kweli lakini kuna ukweli kwa kiasi Fulani kwa sababu niliwahi kushuhudia binafsi eneo moja muhimu sana la serikali siwezi kulitaja na najua yapo maeneo mengi kama hayo ambapo mvua iliponyesha nilishangaa kuona maji yakituama eneo moja na hata kusababisha ofisi niliyokuwa nafanya kazi kuingiliwa na maji , nilitafiti ili nijue hasa tatizo liko wapi , ndipo ilionekana wazi kuna chemba iliyokuwa inapitisha maji taka kuzibwa makusudi ili kuruhusu ujenzi wa majengo hayo ya serikari . Ilinisikitisha sana kama mtaalamu husika wa maji na miundombinu yake na hivyo ndivyo ilivyo katika maeneo mengi na sio sababu kubwa inayoweza kunishawishi kwa sababu ujenzi ukizingatia miundombinu bora ya maji badala ya kujenga ilimradi tatizo la maji taka mijini litapungua au kwisha kabisa.

 Sababu zifuatazo zitatuonyesha jibu la msingi na amini usiamini ndivyo ilivyo

1 . Ongezeko la watu sehemu za mijini

Watu wengi wanapojazana sehemu moja wakiwa katika utafutaji hivyo matumizi ya maji yanakuwa makubwa na maji taka kuwa mengi hii upelekea miundo mbinu hiyo kuelemewa na kiwango cha taka  au maji yanayosafirishwa

 

2. Utupaji taka ovyo

Kila mtu anafahamu yakuwa majiji makubwa yana kabiliana na changamoto kubwa ya uchafu kutokana na mamlaka husika kutowajibika ipasavyo katika utatuzi wa tatizo la uchafu hasa jiji letu la Dar es salaam , swala hili pia huendana na tabia mbaya ya mazoea ya baadhi ya  watu kutupa taka kama za plastiki ovyo , taka hizi husababisha zile chemba muhimu za kupitisha  maji taka kuziba na hivyo maji yanaposhindwa kupita njia iliyopangwa yatatafuta njia mbadala ili yaendelee na safari , hivyo ndivyo watumia barabara na watu wenye shughuri zao mijini wanakutana na kelo ya maji machafu.
3. Uchakavu wa miundo mbinu
   Inawezekana kabisa kuna wakati Fulani miundombinu inayo ruhusu maji taka kupita inatakiwa kufanyiwa matengenezo au kubadili vifaa vya zamani na kuweka vilivyo kuwa vipya ilkusaida mfumo endelevu

NINI KIFANYIKE KATIKA KUTATUA TATIZO HILI ?

Njia zifuatazo ni muhimu katia kushughulika na tatizo

1.Kuwe na ujenzi bora utakao zingatia upitishwaji wa maji safi na maji taka

 Hii itasaidia majitaka kusafiri katika njia zake na hata mafuliko yatakapotokea kusiwe na athari itakayojitokeza maana mifumo husika itaruhusu maji yasituame . ujenzi pia utaenda sambamba na ongezeko la watu , hii ni hesabu za takwimu kwamba miundo mbinu itaweza kubeba maji taka kwa miaka mingi zaidi ikilinganishwa na ongezeko la watu kila mwaka

 

2. Mamlaka maalumu pia izingatie swala la usafi ili kuepisha kuziba kwa chemba za maji taka

Chombo kilichopewa dhamana ya usafi katika majiji makubwa kihakikishe kina weka vifaa maalumu vya kutunzia taka hasa sehemu za mikusanyiko ya watu , cha ajabu unaweza ukatembelea vituo vya dara dara hasa Dar es salaama na usikutane na kitunza uchafu hata kimoja , hii umfanya mtu aliye na taka mkononi kutupa ovyo , jambo hili pia liende sambamba na elimu juu ya usafi , hapa kila mmoja anawajibika kumueleza mwenzake juu ya utunzaji wa mazingira

 

3. kadri inavyowezekana katika taasisi mbali mbali kuwe na mifumo ya ndani ya kutibu maji taka badara ya kusafiri umbali mrefu kwa ajili ya kutibiwa , hii inaweza pia kupunguza gharama na pia inaweza kuzuia kukutana kwa mfumo wa maji taka na ule wa maji safi .mfano wa mifumo ya ndani ni kama pondi za maji taka ,  
 
Asante karibu tena kwa mada nyingine nzuri za kukufanya ubadilike juu ya mazingira na hasa matumizi ya maji

 

 

 

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni