Tafuta katika Blogu Hii

Jumatano, 7 Oktoba 2020

          TUNATOA HUDUMA NA USHAURI KUHUSU MAJI KATIKA NYANJA                   
         ZIFUATAZO 

                                                   Kupima ubora wa maji

                                                   Utafiti wa maji ardhini 

                                                   Uchimbaji wa visima 

                                                   Kuunda mfumo wa matumizi ya maji 
                                                   katika matumizi mbali mbali

                                                   Kuunda mfumo wa maji taka 

                                Kwa ushauri na changamoto za maswala ya maji piga simu 
                                         
                                        0767176463
                                       Email: majiyetu96@gmail.com 
                                                   

       

Jumapili, 9 Aprili 2017

JE UNA UHAKIKA KUWA MAJI YA KISIMA UNACHOTUMIA NI SALAMA ?

Kitaalamu maji yanaweza kuwa safi lakini si salama , bali usalama wa maji yako ni pale yanapoweza kufanyiwa uchunguzi wa kitaalamu na kujua kama hayana wadudu hatarishi hasa bakteria ambao hupatikana kwenye vinyesi vya mwanadamu na wanyama , bakteria hawa husababisha magonjwa ya tumbo na kuhara , unaweza rejea mada zilizopita na kupata ufafanuzi juu ya hao wadudu hatarishi kwenye maji
 






Jinsi ya kupata msaada wa kitaalamu unaweza kuwasiliana nami nakupewa maelekezo jinsi ya kufanya .

Jumapili, 12 Machi 2017

FAHAMU KUHUSU MAJI NA SAYANSI YAKE.BLOG SPOT.COM


Lengo la blogi hii  ni kusaidia na kutoa elimu kwa jamii , hii ni blogi bora ya sayansi Tanzania na Afrika mashariki imeanziswa tarehe 21 /03/2015 ikianza na wasomaji zaidi ya hamsini kwa siku huku ikikua kwa kasi


Blogi hii imejikita katika utafiti na kutatua changamoto  zinazokumba jamii  katika maeneo mbalimbali  ya nchi haswa swala zima la  upatikanaji wa maji safi na salama  ,kutoa ushauri wa kiteknologia kwa watu wenye kampuni vikundi na hata mtu mmoja mmoja wanaojihusisha na biashara ambazo hukutana na changamoto katika swala zima la ubora wa maji au matumizi ya maji kiujumla mara nyingi swala zima la ubora wa maji limekuwa likimulikwa kwa tochi au kutopewa kipaumbele hasa nchi zetu zinazoendelea na watu wengi wanapoona maji yanapatikana kutoka kwenye vyanzo vyao huzania wamemaliza changamoto ,

 lakini ukweli unabaki kuwa maji yanaviambatanishi vingi vinavyoweza kuleta madhara katika afya zetu katika biashara zetu ,viwanda vyetu na ata  katika ujenzi mfano maji yabisi yanaweza kuleta madhara makubwa kwenye mitambo ya kupozea au ya kuchemshia ( boilers), kulika kwa chuma . au chumvichumvi kuganda kwenye kuta za chuma na hivyo kupunguza ufanisi wa mitambo hiyo hii hughalimu makampuni makubwa kiasi kikubwa cha fedha kutatua tatizo au hulazimika kuagiza mitambo mingine  mfano wa mitambo hiyo ni ile inayo tumika kwa ajil ya kufua umeme

 Pia kiafya maji yenye madini tembo yanaweza kusababisha kansa kwa mtumiaji kama yataonekana kwa kiwango kidogo tu pia maji yanaweza kuwa na wadudu hatarishi kiafya , ukuaji wa viwanda na maendeleo ya kiuchumi huchangia kwa kiasi kikubwa katika uchafuzi pale ambapo madini sumu yanapotumika kwenye utengenezaji wa vifaa kama kompyuta , vifaa hivi vinapochakaa , uteketezaji wake unaweza usiwe katika kiwango ambacho ikazuia yasikutane na vyanzo vya maji

Pia tunatoa ushauri juu ya kusafisha na kutibu maji ikitegeme dhumuni lako katika matumizi ya maji hayo

Mfano

Maji kwa matumizi ya kunywa
Maji kwa matumizi ya umwagiliaji
Maji kwa matumizi ya kujengea
Maji kwa matumizi ya viwandani
Maji kwa matumizi ya ufugaji

Pia  wasiliana nasi kwa mahitaji mbali mbali vinavyohusu uchimbaji visima nakadharika


Jumapili, 20 Machi 2016

MAJI BORA KWA AJIRI YA UMWAGILIAJI



Maji ni muhimu sana kwa ajili ya umwagiliaji , katika dunia hii hasa nchi zinazoendelea, ufanisi na ubora katika swala zima la kilimo ni jambo linalotazamwa kwa karibu sana , tumefikia wakati ambapo hatuwezi tena kutegemea mvua ili kufikia kwenye dhima ya uzalishaji bora , hatuwezi tena kutumia jembe la mkono , pia ardhi yenye rutuba ni jambo la kutazamwa kwa karibu sana , watu wengi hukumbuka mambo mengi ya msingi wanapofikilia kuanzisha mradi wa kilimo cha umwagiliaji lakini hawaweki mkazo hasa katika swala zima la ubora wa maji, wengi wetu huamini tu kuwa kama maji yanapatikana eneo husika basi inatosha yatumike katika mradi , jambo hilo si sahii kwa sababu maji yanaviwakilishi vingi ambavyo havihitajiki katika mmea ili uweze kukua , hivyo lengo la blogi hii ni kukupa ushauri wewe mkulima uliye na ndoto za kuvuna mazao yaliyo bora pale utakapo fahamu juu ya ubora wa maji yako , kwani maji yanaweza kuwa na viwakilishi vyenye sumu kali kama vile madini tembo ,unaweza kuwasiliana nami kupitia barua pepe yangu ambayo ni mackthekwembe@gmail.com kwa maelezo zidi .

 

Jumapili, 6 Septemba 2015

KUENEA KWA UGONJWA WA KIPINDUPINDU NA MATUMIZI YA MAJI


Hivi karibuni kumeibuka kwa ugonjwa wa kipindupindu katika jiji la Dar es salaam hasa wilaya ya kinondoni ikishika nafasi ya kwanza kwa kuwa na wagonjwa wengi , ugonjwa huu husababishwa na bacteria anayeitwa vibrio  cholerae , bacteria huyu hupatikana kwenye kinyesi cha binadamu , hivyo ili upate ugonjwa huu ni lazima utakuwa umekula kinyesi pasipo kujua pia ugonjwa huu huenezwa na mawakala wa uchafu hapa nazungumzia mdudu anayeitwa nzi ambaye hupenda kusogelea maeneo machafu hasa yenye vinyesi vya wanyama , huwenda ulikula tunda ambalo halikuoshwa ipasavyo au chakula ambacho hakikuhifadhiwa vizuri hivyo nzi mawakala wakatua kwenye chakula na kuacha vimelea vya magonjwa , lakini kikubwa zaidi matumizi ya maji ambayo si salama kwa kunywa , niliwai kutembelea baadhi ya maeneo ya jiji nikiangalia au kukagua ni kipi kisababishi cha ugonjwa huu wa kipindupindu yapo mengi niliyojifunza lakini kikubwa hasa ni swala zima la mazingira machafu katika maeneo ya nayozunguka nyumba za watu au sehemu za kibiashara kama sokoni




 

SABABU ZIFUATAZO ZILINIFANYA KUANDAA MADA HII KAMA KISABABISHI

 

1.Miundombinu mibovu ya mfumo wa maji taka na maji safi

Jambo hili nimewahi kuliongelea sana , miundombinu chakavu ya maji taka usababisha maji taka kukutana na yale yaliyokuwa safi , uwenda ni yale yaliyotibiwa na dawasco au visima vifupi ambapo watu wamekuwa wakitumia maji hayo ya visima vifupi wakijua ni chemichemi kumbe ni kuvilia ndani kwa ndani kwa maji taka lakini hili linaenda sambamba na ukosefu wa vyoo bora katika baadhi ya maeneo , kuna maeneo ukiingia chooni unaweza ukagairi kujisaidia hata kama ungebanwa vipi na haja , vyoo chakavu vilivyofikia hatua ya kutapika ni rafiki kwa nzi wa kijani kubeba vimelea vya magonjwa hasa kipindupindu  

 
 

2. uwepe wa maji taka karibu na makazi ya watu

Kuna maeneo mengi sana katikati ya jiji la Dar es salaam ambapo ni kawaida kukuta maji machafu yakituama kandokando ya makazi ya watu huku kukiwa na shughuli mbalimbali zikiendelea kama huduma ya vyakura maarufu kama mama ntilie ,hii pia ni hatari kwa watoto wadogo ambao wakati mwingine huona maji hayo kama ni sehemu tu ya michezo yao , huenda wasifikie hatua ya kuyatia kinywani lakini uwezekano wa kugusana nayo mikononi ni mkubwa hivyo wazazi nao wasipokuwa makini mtoto anaweza kula kitu kingine bila ya kunawa mikono na kusababisha kupata ugonjwa , sababu hii inaweza kuwa ya msingi kwa sababu takwimu zimeonyesha kuwa miongoni mwa wagonjwa watoto wamekuwa wengi ukilinganisha na idadi ya watu wazima

 

3 .watu kutozingatia kanuni za afya asa usafi binafsi , mfano kula chakula bila kunawa vizuri , kunywa maji yasiyotibiwa au kuchemshwa , pia kama nilivyosema kuhusu watoto ambao awapatiwi uangalizi wa kutosha kutoka kwa wazazi wanapokuwa katika michezo au katika maswala mazima ya ulaji

 

4. mkusanyiko mkubwa wa watu katika eneo moja ,

Hapa ndipo chanzo cha ugonjwa , kukua kwa kasi kwani utagundua nyumba moja ya kupangisha inaweza kuwa na watu wengi au kukaribiana bila nafasi kati ya nyumba na nyumba hivyo unaweza kuona maeneo hayo maarufu kama uswailini , wakati mwingine uwezi kutofautisha kuwa choo Fulani ni cha nyumba hipi , mifumo ya maji taka mara zingine huingiliana kati ya nyumba na nyumba  kiasi kwamba tabia za baadhi ya watu kutozingatia kanuni za afya upelekea kupatwa na ugonjwa , lakini kwa sababu watu wamekusanyika eneo moja ni rahisi sana kwao kuambukizana , hivyo ni vizuri watu wakajaribu kuishi katka maeneo yenyempangilio wa makazi bora unaoleta maana ya kuishi , mfano mzuri ni wilaya ya ilala ambapo si mara chache sana hupatwa na kipindupindu ,ingawa pia yapo maeneo hatarishi lakini maeneo mengi yamepangilika kimakazi  

 

NINI KIFANYIKE KATIKA KUKABILIANA NA UGONJWA HUU HATARI

Katika kutatua au kupambana na tatizo hili kiuna makundi ya kijamii mashirika binafsi na serikali

1 kijamii

   Swala la usafi wa mazingira linaanza na mtu mmoja mmoja , hasa katika ngazi ya kifamilia , tuache kuwa wavivu wa kukemea au kusemana kuhusu usafi katika maeneo yetu tunayoishi , pia tuache dhana ya kuilaumu serikali bila kufanya sehemu yetu, kama mwanajamii tunawajibu wa kulinda miundombinu ya maji , wapo watu hukata kwa makusudi mipira ya kusambazia maji safi ili ajinufaishe wao , si gharama pekee itakayoingia serikali kufanya matengenezo bali itapelekea kuingiliana kwa mifumo ya maji safi nay ale ya maji taka

 

2 serikali au sekta zisizo rasimi nazo zinaweza kuchangia kuenea kwa ugonjwa kwa namna moja au nyingine , mfano yapo maeneo ambapo hakuna ufatiliaji juu ya miundombinu chakavu inayopitisha maji safi na maji taka ili kujua wapi kuna mipasuko inayo sababisha maji yawe na vimelea vya ugonjwa , hivyo sampuli za maji zichunguzwe kila baada ya mda Fulani kujua kama kuna uchafuzi wa maji au la

Pia mamlaka husika kama wizara ya afya inajukumu kubwa la kuhakikisha elimu ya kutosha inawafikia watu ili wawe na mitazamo mizuri kuelekea afya na mazingira yao.

 

Jumapili, 16 Agosti 2015

CHANGAMOTO ZA MAJI TAKA KATIKA MAJIJI YANAYOKUWA


MAJI TAKA

Maji taka ni yale maji yaliyogusana na uchafu au kitu kisichohitajika kwenye maji , yakihusisha mkusanyiko kutoka mahali tofauti tofauti mfano nyumbani , maji yaliyotumika kuogea ,kufulia , kuoshea viombo na wakati mwingine yakihusishwa na uwepo wa vinyesi , pia maji haya yanaweza kutoka viwandani au kwenye taasisi mbalimbali .

Mkusanyiko wote wa maji haya taka hukutana katika bomba moja kubwa ambalo litasafilisha kuelekea kwenye kumwagwa au kusafishwa na kutibiwa ili yawe katika kiwango kisicholeta madhara kwenye mazingira

Kumekuwapo na changamoto juu ya haya maji taka hasa sehemu za  mijini,uwenda hata wewe ukawa mmojawapo kati ya wale waliokutana na kero ya kuona au hata kukanyaga maji haya machafu wakati ukiwa katika matembezi ,

Maji haya taka ni hatari hasa pale yanapokutana na mfumo wa maji safi ,ambapo  mipira ya kusambazia maji safi inaweza kupasuka hivyo ikapelekea athari kubwa kwa watumiaji    


 

SABABU ZA MAJI TAKA KULETA KELO MIJINI

Hapa kuna sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili sahemu za mijini ingawa wapo wanasiasa wanaodai kuwa inatokana na ujenzi unaondelea kila kukicha katika miji mikubwa hasa ujenzi wa majengo marefu , sitaki kusema sio kweli lakini kuna ukweli kwa kiasi Fulani kwa sababu niliwahi kushuhudia binafsi eneo moja muhimu sana la serikali siwezi kulitaja na najua yapo maeneo mengi kama hayo ambapo mvua iliponyesha nilishangaa kuona maji yakituama eneo moja na hata kusababisha ofisi niliyokuwa nafanya kazi kuingiliwa na maji , nilitafiti ili nijue hasa tatizo liko wapi , ndipo ilionekana wazi kuna chemba iliyokuwa inapitisha maji taka kuzibwa makusudi ili kuruhusu ujenzi wa majengo hayo ya serikari . Ilinisikitisha sana kama mtaalamu husika wa maji na miundombinu yake na hivyo ndivyo ilivyo katika maeneo mengi na sio sababu kubwa inayoweza kunishawishi kwa sababu ujenzi ukizingatia miundombinu bora ya maji badala ya kujenga ilimradi tatizo la maji taka mijini litapungua au kwisha kabisa.

 Sababu zifuatazo zitatuonyesha jibu la msingi na amini usiamini ndivyo ilivyo

1 . Ongezeko la watu sehemu za mijini

Watu wengi wanapojazana sehemu moja wakiwa katika utafutaji hivyo matumizi ya maji yanakuwa makubwa na maji taka kuwa mengi hii upelekea miundo mbinu hiyo kuelemewa na kiwango cha taka  au maji yanayosafirishwa

 

2. Utupaji taka ovyo

Kila mtu anafahamu yakuwa majiji makubwa yana kabiliana na changamoto kubwa ya uchafu kutokana na mamlaka husika kutowajibika ipasavyo katika utatuzi wa tatizo la uchafu hasa jiji letu la Dar es salaam , swala hili pia huendana na tabia mbaya ya mazoea ya baadhi ya  watu kutupa taka kama za plastiki ovyo , taka hizi husababisha zile chemba muhimu za kupitisha  maji taka kuziba na hivyo maji yanaposhindwa kupita njia iliyopangwa yatatafuta njia mbadala ili yaendelee na safari , hivyo ndivyo watumia barabara na watu wenye shughuri zao mijini wanakutana na kelo ya maji machafu.
3. Uchakavu wa miundo mbinu
   Inawezekana kabisa kuna wakati Fulani miundombinu inayo ruhusu maji taka kupita inatakiwa kufanyiwa matengenezo au kubadili vifaa vya zamani na kuweka vilivyo kuwa vipya ilkusaida mfumo endelevu

NINI KIFANYIKE KATIKA KUTATUA TATIZO HILI ?

Njia zifuatazo ni muhimu katia kushughulika na tatizo

1.Kuwe na ujenzi bora utakao zingatia upitishwaji wa maji safi na maji taka

 Hii itasaidia majitaka kusafiri katika njia zake na hata mafuliko yatakapotokea kusiwe na athari itakayojitokeza maana mifumo husika itaruhusu maji yasituame . ujenzi pia utaenda sambamba na ongezeko la watu , hii ni hesabu za takwimu kwamba miundo mbinu itaweza kubeba maji taka kwa miaka mingi zaidi ikilinganishwa na ongezeko la watu kila mwaka

 

2. Mamlaka maalumu pia izingatie swala la usafi ili kuepisha kuziba kwa chemba za maji taka

Chombo kilichopewa dhamana ya usafi katika majiji makubwa kihakikishe kina weka vifaa maalumu vya kutunzia taka hasa sehemu za mikusanyiko ya watu , cha ajabu unaweza ukatembelea vituo vya dara dara hasa Dar es salaama na usikutane na kitunza uchafu hata kimoja , hii umfanya mtu aliye na taka mkononi kutupa ovyo , jambo hili pia liende sambamba na elimu juu ya usafi , hapa kila mmoja anawajibika kumueleza mwenzake juu ya utunzaji wa mazingira

 

3. kadri inavyowezekana katika taasisi mbali mbali kuwe na mifumo ya ndani ya kutibu maji taka badara ya kusafiri umbali mrefu kwa ajili ya kutibiwa , hii inaweza pia kupunguza gharama na pia inaweza kuzuia kukutana kwa mfumo wa maji taka na ule wa maji safi .mfano wa mifumo ya ndani ni kama pondi za maji taka ,  
 
Asante karibu tena kwa mada nyingine nzuri za kukufanya ubadilike juu ya mazingira na hasa matumizi ya maji

 

 

 

 

Jumapili, 9 Agosti 2015

FAHAMU KUHUSU ALGAE FLOC


Ni dawa inayotumika katika sayansi ya kutibu maji , iliyotengenezwa kutokana na vijidudu vinavyoitwa algae ,algae ni miongoni mwa viumbe hai vyenye ukijani kama majani

Wakati maji yamepitia njia tofauti tofauti ya usafishwaji    .Kazi moja kubwa ya algae floc ni kusafisha maji ambayo yamejumuisha taka ndogo sana ambazo zilifanikiwa kupenya kupitia kwenye machujio , taka zote zenye umbo dogo hukusanywa na algaefloc mbayo hutokeza mabonge ambayo mwisho huzama chini kwa nguvu ya mvutano tayari kuondolewa nje ya tanki kwenda kutupwa kama uchafu